KUTUMIA KONDOMU NA MADHARA YAKE'''

Tokeo la picha la MADHARA YA KONDOMU
Mimi mvulana, mimi ni mwanamme nieleze jinsi ya kutumia kondom ya wanaume?
  • Hakikisha umeangalia mda wa matumizi wa kondom uliyonayo. Kama mda wake (expiry date) wa matumizi umekwisha basi haikufai. Fungua kipakiti chenye kondomu wakati tu ukiwa tayari kuitumia. Bila hivyo yale mafuta mafuta maalum kwenye kondomu yatakauka.
  • Unapofungua pakiti kuwa mwangalifu usiipasue, au kuitoboa wala kuiharibu kondom yenyewe. Ikipasuka itupilie mbali na uchukue nyingine.
  • Kondomu huwa zimesokotwa na kuwa kama duara. Kuivaa, ile sehemu ya mafuta mafuta inapaswa kuwa nje.
  • Hivyo basi ivae kwa kuikunjua kuanzia kwenye ncha (kichwa)cha uume.
  • Ishike sehemu ya chuchu ya kondomu kwa kutumia dole gumba na kidole chako cha kwanza ili kutoa hewa kutoka sehemu hiyo, ili manii yahifadhiwe mahali hapo pale yatakapotoka.
  • Sasa Endelea kuishikilia kondom kwa mkono mmoja. Kwa kutumia mkono wa pili ikunjue hadi kufikia kwenye mavuzi yaani kwenye shina la uume. Kama mtumiaji hajatahiriwa anapaswa kuvuta lile govi la uume wake kabla ya kuvaa kondomu. Kama kondomu haina kilainishi cha kutosha, vilainishi au majimaji (kama vile silicone, glycerine, au K-Y jelly) vyaweza kuongezwa kwa nje. Tahadhari mafuta kama yale ya kupikia, ya kujipaka mwilini kama kama vile Vaseline hayafai kutumiwa kama kilainishi.
  • Baada ya kufanya mapenzi kondomu inapaswa kuvuliwa kwa njia sahihi pia. Baada tu ya kufika kilele na kutoa manii, mwanaume anapaswa kuutoa uume wake kutoka ukeni, kabla haujalegea kabisa, kwani akichelewa huenda kondom ikatumbukia ukeni mwa mwanamke. Kisha ashikilie kondomu kutoka shinani mwa uume na kuivua taratibu pasi na manii kumwagika.
  • Unaweza kuifunga kondom kwenye karatasi na kuitupa kwenye choo cha shimo
  • Usitupe kondom kwenye hooni cha kupiga maji kwani huenda ikatatiza utendaji kazi wa choo hicho.
  • Tumia kondom nyengine kwa kila tendo jengine la kujamiana. Tumia kondom kila wakati unapofanya mapenzi.
  • 0765203999

No comments:

Powered by Blogger.