Sababu za wanaume kupenda wake za watu

Kumekuwa na tabia ya wanaume wengi kutaka kuingia katika mapenzi  na wanawake mambo tayari wameshaolewa na hivyo hivyo kwa mabinti kutaka kuwa  na mahusiano na wanaume za watu bila kuogopa kuwa kitu hicho kinaharibu mahusiano ya ndoa ya watu hao au kuvunja familia kabisa.

Kwa bahati mbaya zaidi  kwa maisha ya sasa hivi kuhusu mahusiano unaweza kukutana  na mwanamke naye licha ya kwamba ameolewa lakini naye anajihisi kumpenda mwanaume huyo na  sababu kubwa huwa ni kwamba anakuwa  hapati kile ambacho alikitarajia kwenye ndoa yake. Na hi uwaweka wengi katika njia panda, lakini sababu kubwa ya watu kutembea na watu waliopo katika ndoa huwani :-.
PENZI LA DHATI
Baadhi ya wanaume si kwamba wanaonyesha kuwa wao hawajatulia kwa kuwatokea wake za watu. Baadhi yao penzi la dhati walilonalo dhidi ya wale ambao wameshaingia kwenye ndoa ndilo huwasukuma kufanya hivyo.
Wanachokifanya wao ni kueleza hisia zao bila kujali kuwa, mlengwa ana mtu au laa. Ndiyo maana mtu huyo anaweza kuwa anajua ukweli kwamba fulani ni mke wa mtu lakini kwa kuwa anaamini huyo ndiye wake, analazimika kujaribu zali.
Siyo dhambi kueleza hisia zako lakini ndugu yangu kama unajua kabisa huyo uliyempenda yuko ndani ya ndoa yake au ana mpenzi wake, pambana na hisia zako. Jizuie kwani kumpa usumbufu mke wa mtu ni kujitafutia matatizo bure.
HAKUNA GHARAMA
Baadhi ya wanaume wanawatokea wake za watu kwa kuwa hawatapata usumbufu wa pesa za matumizi, vocha, mavazi na vitu vingine. Wao wanaamini watakuwa wanatoa penzi tu lakini mambo mengine mwenye mke atahudumia.
Lakini wengine wanataka kuanzisha uhusiano na wake za watu kimaslahi. Kwamba mwanaume anaweza kuona mwanamke flani ameolewa na mwanaume mwenye nazo lakini mke anaonekana kutopata penzi analolihitaji. Yeye anatupa ndoano, akiamini akimridhisha kimapenzi, atakuwa anahongwa yeye na maisha yake yatakuwa poa.
Tahadhari. Kama unatokea kumpenda mke wa mtu ili umchune au ili kukwepa kugharamia, tamaa yako hiyo itakuponza. Acha utegemezi, mwanaume aliyekamilika ni yule mwenye uwezo wa kumtunza mtu anayempenda, usikimbie majukumu na kutaka vya mteremko. Kumbuka wengi walioingia kwenye uhusiano na wake za watu kwa tamaa za pesa na mali, yamewakuta makubwa.
USUMBUFU HAKUNA

No comments:

Powered by Blogger.