SIMULIZI MPYA: TANGA RAHA 04
ILIPOISHIA
Xaviena akazidi kukicheza kiuono chake jambo lililo wafanya mapaparazi kila mmoja kuielekezea kamera yake kwa Xaviena na kuwaacha wengine walio kua wakionekana si lolote wala si chochote mbele ya Xavienea
“Karibuni mukae”
Eddy akawa wa kwanza kumtazama mwanamke anaye mkaribisha wakae kwenye viti vyoa, hakuamini kumuona Olvia Hitler akiwa ndio mwenzao, katika meza hiyo nyenye viti vinne, jambo lililo ikatisha furaha yote ya Eddy.
Xaviena akazidi kukicheza kiuono chake jambo lililo wafanya mapaparazi kila mmoja kuielekezea kamera yake kwa Xaviena na kuwaacha wengine walio kua wakionekana si lolote wala si chochote mbele ya Xavienea
“Karibuni mukae”
Eddy akawa wa kwanza kumtazama mwanamke anaye mkaribisha wakae kwenye viti vyoa, hakuamini kumuona Olvia Hitler akiwa ndio mwenzao, katika meza hiyo nyenye viti vinne, jambo lililo ikatisha furaha yote ya Eddy.
ENDELEA
Olvia Hitler akaachia tabasamu lililo mtatiza sana Eddy. Kwenye maisha yake hakutarajia kukutana na Olvia. Ajali waliyo ipata muda mchache ulio pita, chanzo ni Olvia Hitler. Taratibu Rahma akageuza uso wake na kumtazama mwanadada huyo. Rahma mdomo ukambaki wazi, kwa wasiwasi ulio mtawala akajikuta akikaa kwenye kiti huku akiendelea kumtazama Olvia.
“Shikamoo”
Xaviela alimsalimia Olvia na pasipo kujua ni kitu gani kinacho endelea kati ya wazazi wake na mwana dada huyo.
“Marahaba, yule ni pacha wako?”
“Ndio ni pacha mwezangu”
“Mumefanana kwa kweli. Naamini wazazi wako wanafurahia kwa kuwapata nyinyi”
“Nashukuru sana”
Xaviela alizungumza huku naye akikaa. Baada ya shangwe za mashabiki kuisha, taratibu watu wote wakaka kwenye viti vyao. Ukimya kwenye meza hii aliyo kaa Eddy pamoja na Olvia Hitler, ukatawala.
“Wewe kwa nini hukushiriki mashindano haya kama mwenzako?”
Swali la Olvia Hitler, likamfanya Eddy na Shamsa kumtazama Olvia ambaye wana mfahamu vizuri.
“Ahaa mimi sipendelei sana maswala hayo ya urembo.”
“Wewe una pendelea nini?”
“Napendelea sana maswala ya ngumi ngumi na ikiwezekana huko baadaye nije kuwa jasusi hatari wa kike”
“Xaviela”
Shamsa aliita huku akimtazama Xaviela kwa macho makali, ikiwa ni ishara ya kumfanya asiendelee kuropoka ropoka.
“Ila kazi ya ujasusi ni ngumu sana?”
“Yaa ndio naipendelea sana”
Xaviela wala hakujali onyo alilo pewa na mama yake.
“Inabidi wazazi wako wakufanyie mpango wa kuingia kwenye vitengo ambavyo vitakufanya uwe jasusi mzuri”
“Naamini wana sikia. Eti baba utanitafutia ehee?”
“Ndio mwanangu”
Eddy alijibu kwa unyonge huku akimtazama Olvia kwa macho makali sana, yaliyo jaa hasira na uchungu ndani yake.
“Unaitwa Xaviela ehee?”
“Ndio naitwa Xaviela na pacha wangu anaitwa Xaviena”
“Ahaa….sawa sawa. Jitahidi kukamilisha ndoto zako”
“Nitafanya hivyo. Wewe una itwa nani?”
“Olvia, Olivia Hitler”
“Waoo jina ni zuri.”
“Nashukuru sana Xaviela, hata nyinyi majina yenu ni mazuri sana. Wazazi wenu hawajakosea kuwaita hivyo”
“Olvia tafadhali una weza kumuacha mwanangu?”
Eddy alizungumza kwa sauti ya ukali na ya chini chini ambayo wao wanne tu ndio waliweza kuisikia. Jambo hilo likamshangaza sana Xaviela.
“Kuna tatizo mimi kuzungumza na mwanao?”
“Sihitaji uzungumze na wanangu na laiti kama ningefahamu nina kaa na wewe kwenye hii meza wala nisinge thubutu kukalisha makalio yangu hapa”
“Hahaa Eddy. Umekuwa sasa hembu acha hayo mambo yako”
Taratibu Shamsa akapitisha mkono wake chini na kumshika Eddy anaye tetemeka mikono yake kwa hasira kali sana.
“Baba ni nini kinacho endelea?”
“Xaviela tulia”
“Siwezi kutulia mama. Inakuwaje baba ana mfokee dada wa watu?”
Jicho alilo tazamwa Xaviela na baba yake, likamfanya akae kimya huku akitambua kwamba baba yake hayupo sawa.
“Jamani hii ni siku nzuri sana kwenu. Mtoto wenu anakwenda kuchukua taji la miss Tanga. Basi tofauti zetu tuziweke pembeni na tumuunge mkono”
Olvia Hitler alizungumza huku akitabasamu, tabasamu la kinafki lililo mfanya Eddy kushusha pumzi na kuliweka vizuri koti la suti yake. Mashindano yakazidi kupamba moto huku washikiri wakizidi kuchuana vikali. Olvia akanyanyuka kwenye kiti chake na kuanza kutembea kuelekea chooni.
“Nina kuja”
Eddy alizungumza huku naye akinyanyuka kwenye kiti chake.
“Baba Xaviela uwe makini”
“Usijali”
“Mama baba ana kwenda wapi?”
“Chooni”
“Mbona anakwenda mara baada ya Olvia kunyanyuka. Hembu mama niambieni ni nini kinacho endelea?”
“Ni historia ndefu mwanangu. Ila tuendelee kutazama”
“Mama nitaendeleaje kutazama ikiwa wazazi wangu nyinyi hamupo sawa. Hembu kuweni wawazi basi mama”
“Xaviela hembu nipe basi nafasi ya kutafakari kichwani mwangu”
Rahma alizungumza huku akitazama jinsi Eddy anavyo tokomea kwenye eneo hilo la ukumbini. Eddy akamkuta Olvia Hitler akiwa amesimama nje ya vyoo vya kike huku akivuta sigarete.
“Kumbe Eddy bado huja kua kiakili?”
Olvia alizungumza huku akitoa fumba zito la moshi puani mwake.
“Umerudi kufanya nini kwenye maisha yangu?”
“Kwenye maisha yako. Nimekufwata kwako, au nimekuuliza chochote juu ya familia yako?”
“Olvia tafadhali kaa mbali sana na familia yangu. Sitaki siku hata moja uwasogelee wanangu. Nitakufanya kitu ambacho hujawahi kufanywa kwenye maisha yako”
“Mimi, wewe unifanye kitu ambacho sijafahi kufanywa? Eddy umenisahau mimi ni nani eheee?”
Olvia Hitler alizungumza huku macho yake yakibadilika badilia rangi ya mboni zake na kumfanya Eddy kuzidi kujawa na uwoga japo ana jikaza kishujaa.
“Potea mbele ya macho yangu kabla sijakusambaratisha.”
Olvia Hitler alizungumza kwa sauti yenye mitetemo kama ya radi. Eddy hakutamani kabisa akumbane na matatizo aliyo wahi kusababishiwa na Olvia Hitler. Akarudi ukumbini huku jasho likimwagika usoni mwake.
“Baba nini kimekupata?”
“Hakuna kitu?”
“Mmm!! Baba una nidanganya, tupo pembezoni mwa fukwe za habari. Inakuwaje una mwagikwa na jasho kiasi hicho ikiwa eneo hili lina upepo wa kutosha?”
“Xaviela una maswali mengi, hembu tusubiri matokeo ya dada yako”
“Mmmmm”
Olvia Hitler akarudi eneo hilo huku uso wake ukiwa umetawaliwa na tabasamu pana sana. Kitendo cha Xaviena kuwaona wazazi wake wakiwa wamekaa meza moja na Olvia, akazidi kujawa na ujasiri. Hatua wanayo kwenda hivi sasa ni ya mwisho kabisa katika mtanange huu. Hatua ya kuulizwa maswali ya hapo kwa hapo ina hofiwa na kila mshikri kwani unaweza ukawa ume kamilika kwenye kila idara ya urembo, ila eneo hilo likakupunguzia maksi.
‘Lazima nishinde, nimemla ng’ombe mzima kwa nini nishindwe kwenye mkia?’
Xaviena alizungumza huku akijiamini sana.
“Asha asha”
“Beee”
“Huu ndio wakati wa mwisho, utamuachia yule mpuuzi aweze kushinda kirahisi hivi?”
Khadija alizungumza huku akimnong’oneza Asha rafiki yake wa karibu na wote wapo kwenye kinyang’anyiro hichi cha urembo.
“Ile dawa aliyo isema mtaalamu ipo wapi?”
Asha aliuliza huku akimtazama Khadija usoni mwake. Siku kadhaa zilizo pita waliweza kumuita mganga wa kienyeji kambini kwao na akawakabidhi dawa ambayo endapo mmoja wao atafanikiwa kumshika nayo mkono mtu waliye kusudia kumshinda basi, mtu huyo ata hudhurika kwa kuto kuweza kuona tena.
“Ninayo hapa”
“Hembu naiomba”
Asha na Khadija wakasogea pembeni, eneo ambalo hakuna mtu ambaye ana weza kuwaona wakifanya uhalifu wao. Asha akajipaka dawa hiyo ya unga unga mkononi mwake. Kisha akamfwata Xaviena sehemu aliyo simama.
“Xaviena ninaweza kuzungumza na wewe japo kwa dakika hii moja”
Asha alizungumza kwa sauti ilio jaa upole na ustarabu mkubwa sana hadi Xaviena akabaki ameshangaa kwani siku zote Asha amekuwa ni mtu wa vitimbwi kwake.
“Zungumza”
“Unajua mimi ni binadamu. Kuna mambo mengi sana ambayo nimekufanyia, leo ni siku ya mwisho na hakika nisipo weza kukuomba msamaha nitakuwa nime kukosea”
Asha alizungumza kwa upole japo moyoni mwake hamaanishi hicho kinacho mtoka mdomoni mwake.
“Asha leo umekubwa na nini?”
“Kwa nini Xaviena?”
“Sijui kwa nini una niomba msahaha ikiwa ulikiri kwa kinywa chako kwamba una nichukia”
“Xaviena hembu tuachane na hayo yalyo pita. Nakuomba sana uweze kunisamehe mpenzi”
Xaviena akashusha pumzi huku akimtazama Asha.
“Sawa mimi sina shida na wewe. Natambua baadhi ya mambo ulikuwa una yafanya kutokana na wivu, ila siri moja kubwa katika maisha ambayo nakuomba uwe nayo popote utakapo kwenda. Hakikisha kwamba una jibidiisha sana. Hakuna mafanikio yanao kuja pasipo juhudi, wivu pasipo jitihada rafiki yangu hakuna kitu”
“Nashukuru sana Xaviena, hakika sijawahi kukuatana na mwanamke mwema na mkarimu kama wewe”
Asha alizungumza huku akimpa mkono Xaviena, aliye utazama kwa sekunde kadhaa huku akiwa na wasiwasi na mkono huo.
“Nisamehe rafiki yangu”
Asha aliendelea kumshahiwishi Xaviena huku akimpa mkono. Taratibu Xaviena akaupokea mkono huo na wakakumbatiana. Warembo wengine wakapiga makofi, taratibu wakaachiana na huku kila mmoja akiwa na tabasamu pana usoni mwake.
Kitu kilicho mshangaza Asha ni kuto kuona dalili yoyote kwa Xaviena. Hadi kipengele cha kuulizwa maswali kinaanza Xaviena bado yupo vizuri kabisa.
“Mbona kama dawa haifanyi kazi?”
Asha alimuuliza Khadija kwa kumnong’oneza huku wakimsikiliza mshiriki mwezao jinsi anavyo hojiwa na majaji jukwaani.
“Hata mimi nina shangaa, kwa maana mtaalamu alisema tukimshika tu basi ataanguka”
Hadi wana baki Asha na Xaviena kwenye eneo walilopo, hapakuwa na dalili yoyote ya Xaviena kuanguka au kuudhurika kwa mbinu za kishirikina walizo zitumia. Asha akaitwa jukwaani na akahojiwa maswali yake kisha ikafwatia zamu Xaviena.
Xaviena akiwa amevalia gauni refu la rangi ya maziwa huku, likitawaliwa na vimeto meto vya kung’ara, akaanza kukatiza jukwaani huku akitembea kwa mwendo wa kuvutia sana. Shangwe zikazidi kurindima ukumbi mzima. Xaviela akakabidhiwa maiki, akawapungia mashabiki wake mkono huku akisubiria swali kutoka kwa jaji aliye andaliwa kuuliza maswali.
“Xaviela Eddy, nianze na swali kwenye upande wa michezo. Tutajie refaa aliye chezesha fainali za kombe la dunia mwaka 2002. Na ni timu gani ziliingia fainali katika kombe hilo mwaka 2002”
Swali hilo likazua minong’ono mingi ukumbini kwani wengi wao wana hisi ni swali gumu. Xaviena akatabasamu huku akiwatazama wazazi wake pamoja na dada yake. Gafla akaanza kuhisi kizunguzungu kikali sana huku macho yake yakianza kutawaliwa na giza. Akajaribu kusimama wima ila akashindwa na kujikuta akianguka chini mzima mzima na kufanya watu wote ukumbini kujawa na taharuki kubwa.
ITAENDELEA
Olvia Hitler akaachia tabasamu lililo mtatiza sana Eddy. Kwenye maisha yake hakutarajia kukutana na Olvia. Ajali waliyo ipata muda mchache ulio pita, chanzo ni Olvia Hitler. Taratibu Rahma akageuza uso wake na kumtazama mwanadada huyo. Rahma mdomo ukambaki wazi, kwa wasiwasi ulio mtawala akajikuta akikaa kwenye kiti huku akiendelea kumtazama Olvia.
“Shikamoo”
Xaviela alimsalimia Olvia na pasipo kujua ni kitu gani kinacho endelea kati ya wazazi wake na mwana dada huyo.
“Marahaba, yule ni pacha wako?”
“Ndio ni pacha mwezangu”
“Mumefanana kwa kweli. Naamini wazazi wako wanafurahia kwa kuwapata nyinyi”
“Nashukuru sana”
Xaviela alizungumza huku naye akikaa. Baada ya shangwe za mashabiki kuisha, taratibu watu wote wakaka kwenye viti vyao. Ukimya kwenye meza hii aliyo kaa Eddy pamoja na Olvia Hitler, ukatawala.
“Wewe kwa nini hukushiriki mashindano haya kama mwenzako?”
Swali la Olvia Hitler, likamfanya Eddy na Shamsa kumtazama Olvia ambaye wana mfahamu vizuri.
“Ahaa mimi sipendelei sana maswala hayo ya urembo.”
“Wewe una pendelea nini?”
“Napendelea sana maswala ya ngumi ngumi na ikiwezekana huko baadaye nije kuwa jasusi hatari wa kike”
“Xaviela”
Shamsa aliita huku akimtazama Xaviela kwa macho makali, ikiwa ni ishara ya kumfanya asiendelee kuropoka ropoka.
“Ila kazi ya ujasusi ni ngumu sana?”
“Yaa ndio naipendelea sana”
Xaviela wala hakujali onyo alilo pewa na mama yake.
“Inabidi wazazi wako wakufanyie mpango wa kuingia kwenye vitengo ambavyo vitakufanya uwe jasusi mzuri”
“Naamini wana sikia. Eti baba utanitafutia ehee?”
“Ndio mwanangu”
Eddy alijibu kwa unyonge huku akimtazama Olvia kwa macho makali sana, yaliyo jaa hasira na uchungu ndani yake.
“Unaitwa Xaviela ehee?”
“Ndio naitwa Xaviela na pacha wangu anaitwa Xaviena”
“Ahaa….sawa sawa. Jitahidi kukamilisha ndoto zako”
“Nitafanya hivyo. Wewe una itwa nani?”
“Olvia, Olivia Hitler”
“Waoo jina ni zuri.”
“Nashukuru sana Xaviela, hata nyinyi majina yenu ni mazuri sana. Wazazi wenu hawajakosea kuwaita hivyo”
“Olvia tafadhali una weza kumuacha mwanangu?”
Eddy alizungumza kwa sauti ya ukali na ya chini chini ambayo wao wanne tu ndio waliweza kuisikia. Jambo hilo likamshangaza sana Xaviela.
“Kuna tatizo mimi kuzungumza na mwanao?”
“Sihitaji uzungumze na wanangu na laiti kama ningefahamu nina kaa na wewe kwenye hii meza wala nisinge thubutu kukalisha makalio yangu hapa”
“Hahaa Eddy. Umekuwa sasa hembu acha hayo mambo yako”
Taratibu Shamsa akapitisha mkono wake chini na kumshika Eddy anaye tetemeka mikono yake kwa hasira kali sana.
“Baba ni nini kinacho endelea?”
“Xaviela tulia”
“Siwezi kutulia mama. Inakuwaje baba ana mfokee dada wa watu?”
Jicho alilo tazamwa Xaviela na baba yake, likamfanya akae kimya huku akitambua kwamba baba yake hayupo sawa.
“Jamani hii ni siku nzuri sana kwenu. Mtoto wenu anakwenda kuchukua taji la miss Tanga. Basi tofauti zetu tuziweke pembeni na tumuunge mkono”
Olvia Hitler alizungumza huku akitabasamu, tabasamu la kinafki lililo mfanya Eddy kushusha pumzi na kuliweka vizuri koti la suti yake. Mashindano yakazidi kupamba moto huku washikiri wakizidi kuchuana vikali. Olvia akanyanyuka kwenye kiti chake na kuanza kutembea kuelekea chooni.
“Nina kuja”
Eddy alizungumza huku naye akinyanyuka kwenye kiti chake.
“Baba Xaviela uwe makini”
“Usijali”
“Mama baba ana kwenda wapi?”
“Chooni”
“Mbona anakwenda mara baada ya Olvia kunyanyuka. Hembu mama niambieni ni nini kinacho endelea?”
“Ni historia ndefu mwanangu. Ila tuendelee kutazama”
“Mama nitaendeleaje kutazama ikiwa wazazi wangu nyinyi hamupo sawa. Hembu kuweni wawazi basi mama”
“Xaviela hembu nipe basi nafasi ya kutafakari kichwani mwangu”
Rahma alizungumza huku akitazama jinsi Eddy anavyo tokomea kwenye eneo hilo la ukumbini. Eddy akamkuta Olvia Hitler akiwa amesimama nje ya vyoo vya kike huku akivuta sigarete.
“Kumbe Eddy bado huja kua kiakili?”
Olvia alizungumza huku akitoa fumba zito la moshi puani mwake.
“Umerudi kufanya nini kwenye maisha yangu?”
“Kwenye maisha yako. Nimekufwata kwako, au nimekuuliza chochote juu ya familia yako?”
“Olvia tafadhali kaa mbali sana na familia yangu. Sitaki siku hata moja uwasogelee wanangu. Nitakufanya kitu ambacho hujawahi kufanywa kwenye maisha yako”
“Mimi, wewe unifanye kitu ambacho sijafahi kufanywa? Eddy umenisahau mimi ni nani eheee?”
Olvia Hitler alizungumza huku macho yake yakibadilika badilia rangi ya mboni zake na kumfanya Eddy kuzidi kujawa na uwoga japo ana jikaza kishujaa.
“Potea mbele ya macho yangu kabla sijakusambaratisha.”
Olvia Hitler alizungumza kwa sauti yenye mitetemo kama ya radi. Eddy hakutamani kabisa akumbane na matatizo aliyo wahi kusababishiwa na Olvia Hitler. Akarudi ukumbini huku jasho likimwagika usoni mwake.
“Baba nini kimekupata?”
“Hakuna kitu?”
“Mmm!! Baba una nidanganya, tupo pembezoni mwa fukwe za habari. Inakuwaje una mwagikwa na jasho kiasi hicho ikiwa eneo hili lina upepo wa kutosha?”
“Xaviela una maswali mengi, hembu tusubiri matokeo ya dada yako”
“Mmmmm”
Olvia Hitler akarudi eneo hilo huku uso wake ukiwa umetawaliwa na tabasamu pana sana. Kitendo cha Xaviena kuwaona wazazi wake wakiwa wamekaa meza moja na Olvia, akazidi kujawa na ujasiri. Hatua wanayo kwenda hivi sasa ni ya mwisho kabisa katika mtanange huu. Hatua ya kuulizwa maswali ya hapo kwa hapo ina hofiwa na kila mshikri kwani unaweza ukawa ume kamilika kwenye kila idara ya urembo, ila eneo hilo likakupunguzia maksi.
‘Lazima nishinde, nimemla ng’ombe mzima kwa nini nishindwe kwenye mkia?’
Xaviena alizungumza huku akijiamini sana.
“Asha asha”
“Beee”
“Huu ndio wakati wa mwisho, utamuachia yule mpuuzi aweze kushinda kirahisi hivi?”
Khadija alizungumza huku akimnong’oneza Asha rafiki yake wa karibu na wote wapo kwenye kinyang’anyiro hichi cha urembo.
“Ile dawa aliyo isema mtaalamu ipo wapi?”
Asha aliuliza huku akimtazama Khadija usoni mwake. Siku kadhaa zilizo pita waliweza kumuita mganga wa kienyeji kambini kwao na akawakabidhi dawa ambayo endapo mmoja wao atafanikiwa kumshika nayo mkono mtu waliye kusudia kumshinda basi, mtu huyo ata hudhurika kwa kuto kuweza kuona tena.
“Ninayo hapa”
“Hembu naiomba”
Asha na Khadija wakasogea pembeni, eneo ambalo hakuna mtu ambaye ana weza kuwaona wakifanya uhalifu wao. Asha akajipaka dawa hiyo ya unga unga mkononi mwake. Kisha akamfwata Xaviena sehemu aliyo simama.
“Xaviena ninaweza kuzungumza na wewe japo kwa dakika hii moja”
Asha alizungumza kwa sauti ilio jaa upole na ustarabu mkubwa sana hadi Xaviena akabaki ameshangaa kwani siku zote Asha amekuwa ni mtu wa vitimbwi kwake.
“Zungumza”
“Unajua mimi ni binadamu. Kuna mambo mengi sana ambayo nimekufanyia, leo ni siku ya mwisho na hakika nisipo weza kukuomba msamaha nitakuwa nime kukosea”
Asha alizungumza kwa upole japo moyoni mwake hamaanishi hicho kinacho mtoka mdomoni mwake.
“Asha leo umekubwa na nini?”
“Kwa nini Xaviena?”
“Sijui kwa nini una niomba msahaha ikiwa ulikiri kwa kinywa chako kwamba una nichukia”
“Xaviena hembu tuachane na hayo yalyo pita. Nakuomba sana uweze kunisamehe mpenzi”
Xaviena akashusha pumzi huku akimtazama Asha.
“Sawa mimi sina shida na wewe. Natambua baadhi ya mambo ulikuwa una yafanya kutokana na wivu, ila siri moja kubwa katika maisha ambayo nakuomba uwe nayo popote utakapo kwenda. Hakikisha kwamba una jibidiisha sana. Hakuna mafanikio yanao kuja pasipo juhudi, wivu pasipo jitihada rafiki yangu hakuna kitu”
“Nashukuru sana Xaviena, hakika sijawahi kukuatana na mwanamke mwema na mkarimu kama wewe”
Asha alizungumza huku akimpa mkono Xaviena, aliye utazama kwa sekunde kadhaa huku akiwa na wasiwasi na mkono huo.
“Nisamehe rafiki yangu”
Asha aliendelea kumshahiwishi Xaviena huku akimpa mkono. Taratibu Xaviena akaupokea mkono huo na wakakumbatiana. Warembo wengine wakapiga makofi, taratibu wakaachiana na huku kila mmoja akiwa na tabasamu pana usoni mwake.
Kitu kilicho mshangaza Asha ni kuto kuona dalili yoyote kwa Xaviena. Hadi kipengele cha kuulizwa maswali kinaanza Xaviena bado yupo vizuri kabisa.
“Mbona kama dawa haifanyi kazi?”
Asha alimuuliza Khadija kwa kumnong’oneza huku wakimsikiliza mshiriki mwezao jinsi anavyo hojiwa na majaji jukwaani.
“Hata mimi nina shangaa, kwa maana mtaalamu alisema tukimshika tu basi ataanguka”
Hadi wana baki Asha na Xaviena kwenye eneo walilopo, hapakuwa na dalili yoyote ya Xaviena kuanguka au kuudhurika kwa mbinu za kishirikina walizo zitumia. Asha akaitwa jukwaani na akahojiwa maswali yake kisha ikafwatia zamu Xaviena.
Xaviena akiwa amevalia gauni refu la rangi ya maziwa huku, likitawaliwa na vimeto meto vya kung’ara, akaanza kukatiza jukwaani huku akitembea kwa mwendo wa kuvutia sana. Shangwe zikazidi kurindima ukumbi mzima. Xaviela akakabidhiwa maiki, akawapungia mashabiki wake mkono huku akisubiria swali kutoka kwa jaji aliye andaliwa kuuliza maswali.
“Xaviela Eddy, nianze na swali kwenye upande wa michezo. Tutajie refaa aliye chezesha fainali za kombe la dunia mwaka 2002. Na ni timu gani ziliingia fainali katika kombe hilo mwaka 2002”
Swali hilo likazua minong’ono mingi ukumbini kwani wengi wao wana hisi ni swali gumu. Xaviena akatabasamu huku akiwatazama wazazi wake pamoja na dada yake. Gafla akaanza kuhisi kizunguzungu kikali sana huku macho yake yakianza kutawaliwa na giza. Akajaribu kusimama wima ila akashindwa na kujikuta akianguka chini mzima mzima na kufanya watu wote ukumbini kujawa na taharuki kubwa.
ITAENDELEA
from Tujifunze Mapenzi https://ift.tt/2zQD9Q6
via
No comments: