FAHAMU KITU HATARI SANA KATIKA MAPENZI NA FAMILIA

WAPENZI wanagombana, ndoa

zinavunjika na familia nyingi zipo kwenye

msoto kwa sababu ya ubinafsi.

Tunazungumza mengi lakini ukweli ni

kwamba endapo kila mmoja atafanikiwa

kuushinda ubinafasi, upendo utashamiri

kila kona.

Ubinafsi una matawi mengi. Mtu

anaposaliti, maana yake ametekwa na

tamaa binafsi. Anashindwa kutambua

kwamba yeye ni mpenzi wa mtu, kwa

hiyo anatakiwa kulinda penzi la

mwenzake. Hajui kama anachokifanya ni

dhuluma ya hali ya juu.

Ukweli ni kwamba unapoanzisha

uhusiano na mtu, maana yake umeamua

kumchagua yeye ndiye amiliki penzi lako.

Kwa hiyo ukienda kulitoa kwa mwingine,

huo ni ubinafsi. Umeingiwa na umimi

kwa kuona kwamba unatoa rasilimali za

ndani ya mwili wako mwenyewe.

Kwa nini ukimfumania mwenzi wako

panachimbika? Ni kwa sababu

alichokitoa kwa mtu mwingine ni chako,

kwa maana hiyo amekutendea dhuluma.

Ndiyo maana ukawa na jeuri ya kupigana

kwa sababu haki yako imetumika ndivyo

sivyo.

Hivyo basi, usaliti ni ubinafsi. Umeingiwa

na jeuri kwamba unacho ndani ya mwili

wako, kwa hiyo unaweza kukitumia bila

kumshirikisha mwenzi wako. Hiyo ni

tabia mbaya mno. Kabla ya kusaliti, fikiria

utakavyoumia pindi utakaposalitiwa.

Kama inauma, ni kwa nini umtende

mwenzako? Je, umemuona yeye hana

moyo? Anza leo kukemea ubinafsi.

Popote pale utakapoona unachukua

nafasi, upinge kwa sababu ni adui

mkubwa mno kwenye mapenzi. Siku zote

usiseme "nipo", sema "tupo".

Unapozunguka, usiwaze "upo",

unatakiwa kuwaza "mpo". Hii itakusaidia

kulinda siti ya mwenzako kila

utakapokwenda. Hakikisha nafasi ya

mwenzi wako haichafuliwi au kutolewa

mkopo. Kama ilivyo kwenye soka,

wachezaji huchezea timu nyingine kwa

mkopo ndivyo na mapenzi ya sasa

yalivyo.

Ni kweli mtu ana mpenzi wake lakini

anavyojieleza anatoa picha kwa muulizaji

kuona kwamba aliyepo si muhimu sana.

Hii husababisha muulizaji aombe kukaa

na baadaye hukaribishwa. Wengi

walikaribishwa kwa mkopo, mwisho

wakawa wamiliki wa jumla.

Kwa nini umwambie huyo mtu kwamba

anaweza kukaa, wakati unajua siti ina

mmiliki wake halali? Kwa porojo za

kitoto, eti mnaambiana mfanye siri.

Kinachosikitisha ni kwamba ukisikia na

mwenzako naye kagawa siti yako kwa

mwingine, macho yatakutoka kwa hasira.

Si wakati wa kuchukia unapotendwa, bali

unatakiwa uache ubinafsi. Haliitwi penzi

bila kuwepo watu wawili. Lazima

uhakikishe unalinda la mwenzako ili na

lako lilindwe. Somo la mkuki kwa

nguruwe kwa binadamu mchungu,

linafundisha kuacha ubinafsi. Mfikirie

mwingine.

Kama ambavyo ubinafsi unavyowatesa

wananchi pale kiongozi mwenye

dhamana kiserikali anaposhindwa

kutimiza majukumu yake na kuamua

kushughulikia shida zake binafsi, huku

akitumia rasilimali za umma, ni kirusi

hatari kila upande.

Baba anapoamua kufuja fedha wakati

anajifahamu anayo familia

inayomtegemea, huo ni ubinafsi.

Anafikiria kutumbua yeye binafsi, wakati

anatakiwa kujenga msingi wa familia.

Anashindwa kujua kwamba fedha

anazotafuta si zake peke yake.

Kama anaona anatakiwa kutumia fedha

zake peke yake, basi hapaswi kujipa

mzigo wa kumiliki familia. Mtu

anapokuwa baba au mama, uamuzi wake

unatakiwa uwe kwa ajili ya wengi.

Kumaliza mshahara kwenye kumbi za

starehe ni ukatili kwa familia hususan

mtoto ambaye hakukuomba umlete

duniani.

Usijidanganye kwamba unajimiliki

mwenyewe. Wewe unamilikiwa na

familia yako, kwa hiyo una deni na

wajibu mkubwa kwa wale wanaohusika.

Kabla ya kwenda nyumba ya kulala

wageni na huyo unayemtamani, fikiria

kwamba unamilikiwa.

Baba au mama, anapokwenda hoteli na

mpenzi wa nje. Akakubali kuvua nguo na

kufanya mapenzi. Ajitambue kuwa

anachezea maisha ya watu wengine.

Kuna maradhi, kwa hiyo unatakiwa uwe

na afya njema ili wanaokumiliki

waendelee kupata huduma yako.

Unafahamu kwamba mapenzi yanaua.

Unaelewa kuwa unaposhindwa kuwa

mtulivu nyumbani, unaiba muda wa

familia yako. Kumbe sasa, fedha siyo zako

ila ni za familia. Unaweza kupata picha

kwamba viungo ni vyako lakini penzi si

lako. Ukilitoa ni wizi, ni dhuluma

iliyopitiliza.



No comments:

Powered by Blogger.