Nifanye Nini Ili Niache Kufikiria Ngono Saa Zote?

Tokeo la picha la hatua za kupunguza hisia
“MIMI hujikuta nikifikiria wasichana saa zote—hata wakati ambapo hawapo,” asema kijana mmoja anayeitwa Michael. “Sielewi. Nyakati nyingine siwezi kukazia fikira jambo lolote!”
Je, wewe hutumia saa nyingi ukiwaza juu ya watu wa jinsia tofauti, kama anavyofanya Michael? Ikiwa ndivyo, huenda ukahisi kana kwamba unapigana vita na akili yako. Fikira za ngono huingia akilini mwako kama jeshi la adui. “Fikira hizo zinaweza kukutawala,” asema Michael. “Zinaweza kukufanya uzunguke njia ndefu ili tu umtupie jicho msichana fulani mrembo, au kutembea-tembea dukani wakati ambapo hukusudii kununua chochote ili tu umtazame mtu fulani kwa ukaribu.”
Hata hivyo, kumbuka kwamba kuwa na hisia za ngono si dhambi. Mungu alimuumba mwanamume na mwanamke wakiwa na uvutano wenye nguvu kati yao, na hakuna ubaya wa kutosheleza tamaa za ngono katika mpango wa ndoa. Kabla ya kufunga ndoa, huenda ukawa na tamaa kali za ngono. Hilo likitokea, usidhani kwamba wewe ni mtu mwovu au kwamba huwezi kuishi maisha safi. Unaweza kudumisha usafi wa kiadili ukiamua kufanya hivyo! Lakini ili ufanikiwe, utahitaji kudhibiti mawazo yako kuhusu watu wa jinsi tofauti. Unaweza kufanya hivyo jinsi gani?
Angalia watu unaoshirikiana nao. Wanafunzi wenzako wakianza kuzungumzia mambo ya ngono, huenda ukataka kuchangia mazungumzo hayo—ili tu usionekane mshamba. Hata hivyo, kwa kweli kushiriki mazungumzo hayo kutafanya iwe vigumu zaidi kwako kudhibiti mawazo yako. Ufanye nini? Usimame tu na kuondoka? Ndiyo, na usione aibu kufanya hivyo! Mara nyingi inawezekana kuondoka pasipo kuonekana “mtakatifu” au kuwafanya wenzako wakucheke.
Epuka kujifurahisha kwa mambo machafu. Bila shaka, haimaanishi kwamba sinema zote, au miziki yote ni mibaya. Hata hivyo, katika ulimwengu wa leo burudani nyingi zimekusudiwa kuamsha tamaa zisizofaa za ngono. Biblia inatoa shauri gani? “Acheni tujisafishe wenyewe kila unajisi wa mwili na roho, tukiukamilisha utakatifu katika kumwogopa Mungu.”) Epuka kabisa burudani zote zinazoweza kuchochea tamaa zisizofaa za ngono.*
Tatizo la Kupiga Punyeto
Vijana fulani hujaribu kupunguza tamaa ya ngono kwa kupiga punyeto. Lakini kufanya hivyo kunaweza kutokeza matatizo makubwa. Biblia inawahimiza Wakristo hivi: “Viueni viungo vya mwili wenu vilivyo duniani kwa habari ya uasherati, uchafu, hamu ya ngono, tamaa yenye madhara, na kutamani.”  Kupiga punyeto ni kinyume kabisa cha ‘kuua hamu ya ngono.’ Kwa kweli, kupiga punyeto huchochea na kukuza hamu hiyo!
Kupiga punyeto kwaweza kukufanya kuwa mtumwa wa tamaa zako.Hatua moja unayoweza kuchukua ili kushinda zoea hilo ni kuzungumza na mtu unayemtumaini. Mkristo aliyekuwa na tatizo la kupiga punyeto kwa miaka mingi anasema hivi: “Laiti ningeweza kupata ujasiri wa kuzungumza na mtu fulani kuhusu tatizo hilo nilipokuwa kijana! Kwa miaka mingi nilisumbuliwa na hisia za hatia, nazo ziliathiri sana uhusiano wangu na wengine, na zaidi ya yote, uhusiano wangu na Yehova.”
Ni nani unayeweza kuongea naye? Mara nyingi ingefaa kuzungumza na mzazi. Au huenda Mkristo mkomavu kutanikoni anaweza kukusaidia. Unaweza kuanza kwa kusema, “Ningependa kuzungumza nawe kuhusu tatizo linalonisumbua sana.”
André aliongea na mzee Mkristo, naye anafurahi kwamba alifanya hivyo. “Mzee huyo alipokuwa akinisikiliza, alilengwa-lengwa na machozi,” André anasema. “Nilipomaliza kuzungumza, alinihakikishia kwamba Yehova ananipenda. Aliniambia kwamba watu wengi wana tatizo kama langu. Aliahidi kwamba atakuwa akizungumza nami mara kwa mara kuona nimefanya maendeleo kiasi gani na kuniletea habari zaidi kutoka katika vitabu vinavyotegemea Biblia. Baada ya kuongea naye, niliazimia kupiga vita zoea hilo—hata ikiwa ningeanguka mara moja moja.”
Mário aliamua kuongea na baba yake, aliyemjali sana na kuelewa hali yake. Hata alikiri mbele za Mário kwamba alipokuwa kijana haikuwa rahisi kwake kushinda zoea hilo. “Nilitiwa moyo sana na mazungumzo hayo ya waziwazi na unyoofu wa baba yangu,” asema Mário. “Nilijiambia, ikiwa alifaulu, hata mimi nitafaulu. Niliguswa moyo sana na mtazamo wa baba yangu hivi kwamba sikujizuia kulia.”
Kama André na Mário, wewe pia unaweza kupata msaada wa kushinda zoea la kupiga punyeto. Hata ukijikuta umetumbukia tena, usikate tamaa! Uwe na hakika kwamba unaweza kushinda vita hivyo.*
Dhibiti Fikira Zako
Mtume Paulo alisema: “Naupigapiga mwili wangu na kuuongoza kama mtumwa.) Vivyo hivyo, huenda wewe pia ukahitaji kujitia nidhamu wakati mawazo yasiyofaa kuhusu watu wa jinsia tofauti yanapoingia katika akili yako. Mawazo hayo yakiendelea, jaribu kufanya mazoezi ya kimwili. Biblia inasema: “Mazoezi ya kimwili ni yenye faida kidogo.” (Kutembea kasi kwa muda au kufanya mazoezi ya kimwili kwa dakika chache kwaweza kukusaidia kuondolea mbali mawazo hayo yasiyofaa.
Zaidi ya yote, usipuuze msaada kutoka kwa Baba yako wa mbinguni. Mkristo mmoja anasema hivi: “Tamaa za ngono zinapoanza kuamka najilazimisha kusali.” Si kwamba Mungu atakufanya uache kupendezwa na watu wa jinsia tofauti. Lakini anaweza kukusaidia kuona kwamba kuna mambo mengine mengi unayoweza kukazia fikira zako.
0765203999

No comments:

Powered by Blogger.